Sunday, 19 June 2016

OZIL ACHUKIZWA NA KAULI YA BOATENG.

Ozil na Boateng.
Mwangi K. Githinji. 

Baada ya mlinzi wa Bayern Munich Jerome Boateng kuwakemea washambulizi wa timu hiyo kutokana na sare yao ya 0-0 dhidi ya Poland, staa wa arsenal Mesut Ozil amejitokeza na kumjibu.

Ujerumani waliambulia sare ya 0-0 kwenye mechi hiyo ya awamu ya makundi jambo ambalo halikumfurahisha mlinzi huyo akisema kuwa kitengo cha timu yao kilikosa maarifa ambayo yangewasaidia kupenyeza safu ya ulinzi ya Poland.

Ozil amemnyamazisha Boateng huku akimpa jibu la utani akimwambia kwamba usemi wake ni maoni tu na kwamba ana ruhusa ya kunena maneno hayo kwa kuwa yeye ni fundi wa kucheza soka la kushambulia.


Kwa sasa timu hiyo inayofunzwa na kocha Joachim Low inaongoza kundi C na watakabiliana na Northern Ireland katika mechi yao ya mwisho.

No comments: