Sunday, 19 June 2016

UCHUNGUZI WA KISA CHA MUME NA MKEWE KUTEKETEZWA NYAMIRA UMEANZISHWA


Polisi wameanzisha uchunguzi wa kisa hicho cha kutamausha

Ben Kirui 

Polisi katika kaunti ya Nyamira wanachunguza kisa ambapo mwanaume mmoja na mkewe walipoteza maisha eneo Mobamba baada ya kushambuliwa na genge la watu wasiojulikana.

Inadaiwa kwamba genge hilo la takriban watu 200 liliingia katika Nyumba ya wawili hao usiku wa kuamkia Jumapili na kuwalazimisha kunywa petroli kabla ya kuwateketeza.

Ocpd wa Nyamira Ricoh Ngare amesema uchunguzi umeanzishwa hasa ikidaiwa kwamba tendo hilo ni la kulipiza kisasi.

Inaarifiwa kwamba wawili hao walihusika katika kutiwa mbaroni kwa mshukiwa mmoja wa wizi ambaye alifariki baada ya kuachiliwa huru kutoka gerezani.
 

No comments: