![]() |
| Mchezaji wa Uhispania na chelsea Pedro. |
Na Mwangi K .Githinji.
Mchezaji wa Uhispania na klabu cha Chelsea Pedro Rodriguez ameomba msamaha
kufuatia kauli yake, alipokiri kwamba hana furaha kwa kukosa
kuchezeshwa kwenye michuano inayoendelea ya yuro na kuwa alikuwa anawazia
kuondoka kutoka kwa michezo hiyo.
Winga huyo wa Chelsea aliingia kama nguvu mpya kwenye mechi
yao ya kwanza na Czech Republic lakini akakosa kupewa nafasi Uhipania
ilipokabiliana na Turkey hivi majuzi.
Licha ya haya kauli
yake ilibadilika pindi tu alipofanya kikao na wanahabari hapo jana akisema
kwamba tayari wamesuluhisha swala hilo na mkufunzi Del Bosque pamoja na
wachezaji wenzake na kulizika kwenye kaburi la sahao.

No comments:
Post a Comment