Monday, 11 July 2016

HALI SI HALI SUDAN KUSINI HUKU WAKENYA NCHINI HUMO WAKIHOFIA MAISHA YAO!!

Maelfu ya watu nchini Sudan Kusini wametoroka makwao
Ben Kirui
Hali nchini Sudan Kusini inazidi kudorora huku maelfu ya watu wakiripotiwa kutoroka makwao kutokana na kuendelea kwa vita.

Jamii ya kimataifa kipitia kwa shirika la IGAD imeapa kwamba haitaruhusu mapigano kuendelea katika taifa hilo changa zaidi barani Afrika.

Wakenya walioko nchini humo wanahofia maisha yao huku wakitaka serikali ya Kenya kuingilia kati kuwaokoa kwani wanajeshi wameanza kushambulia raia.

Nchi ya Uganda imelazimika kufunga mpaka wake na Sudan Kusini. Msemaji wa jeshi la Uganda amesema Uganda imeamua kuchukua hatua hiyo ili kujiweka tayari kuwanasa wale ambao huenda wakachukua fursa ya hali tete nchini Sudan Kusini kuvuruga amani nchini Uganda. 

No comments: