Monday, 29 February 2016

SIMBA WAWILI WATOROKA MBUGA TENA

Ben Kirui

Simba wawili wameonekana hii leo katika barabara ya Bypass karibu na makutano ya barabara ya Ngong hapa jijini Nairobi wiki moja tu baada ya simba wengine kutoroka kutoka mbuga ya taifa ya Nairobi.
Polisi wa trafiki, waliokuwa wakipiga doria katika barabara ya Southern Bypass waliwaona samba hao na kuwapasha habari maafisa wa KWS ambao wameanza operesheni ya kuwatafuta wanyama hao.
Wanyama hao wameonekana wakitembea karibu na ua unaozunguka msitu wa barabara ya Ngong, karibu na kituo cha idara ya misitu ya Kenya (KFS).

No comments: